Ijumaa, 31 Machi 2017

WANANCHI WA KIJIJI CHA SHAURIMOYO WAMALIZA MGOGORO NA MWEKEZAJI


Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dkt. Joel N. Bendera amekabidhiwa hati ya shamba lenye ukubwa wa Ekari 1098 lililokuwa likigombewa na wananchi mali ya mwekezaji Bwana PARU Parvinder Nyotta mwenye Kampuni ya Republic Body Builders LTD wa Kijiji cha Shaurimoyo kwa ajili ya kuwagawia wananchi ili kumaliza mgogoro uliodumu kwa zaidi ya mikaka kumi.

WALIMU HANANG WAKUTANA NA MKUU WA MKOA KUBORESHA ELIMU.


Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dkt. Joel N. Bendera akiongea na Walimu wa Shule ya Sekondari na Msingi wa Wilaya ya Hanang' kwa ajili ya kupeana mikakati ya kuboresha ufundishaji katika shule zao.

WATUMISHI WA UMMA MKOA WA MANYARA WAPATA VITAMBULISHO VYA URAIA




Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dkt. Joel N. Bendera amefanya uzinduzi ofisini kwake  wa kugawa Vitambulisho vya Uraia kwa watumishi wa UMMA Mkoa wa Manyara baada ya Mamlaka ya vitambulisho (NIDA) kukamilisha usajili na uhakiki. 


Alhamisi, 30 Machi 2017

ZIARA YA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA MAJALIWA (Mb) MKOA WA MANYARA





















Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) akiwasili Mkoa wa Manyara na kupokelewa na Katibu Tawala Mkoa Eliakim C. Maswi katika ziara yake ya kikazi ndani ya Mkoa.

Ziara hiyo ilidumu kwa muda wa Siku tano ambapo alitembelea Wilaya zote za Mkoa wa Manyara ambazo ni Halmashauri za Simanjiro, Kiteto,  Mbulu, Hanang' na Babati.

Ona Ziara hiyo hapa